VIJANA WENZANGU MNAPOAMUA KUOA MREMBO WA KIDIGITALI AU BINTI MSOMI KUBALIANA NA YAFUATAYO...√√ - EDUSPORTSTZ

Latest

VIJANA WENZANGU MNAPOAMUA KUOA MREMBO WA KIDIGITALI AU BINTI MSOMI KUBALIANA NA YAFUATAYO...√√


Usasa unatuchanganya ubongo vijana,usasa unatufanya tutumie hela na mda mwingi kwenye mambo yasiyo ya msingi na kusahau mambo ya msingi....√√√
1. Wasichana wengi sasa hawajui kupika,lakini mbali na kupika hawajui hata kuosha vyombo wala ,mabint wa kidigitali wanajali sana miili yao kuliko maisha yao,mda wote wanataka kuona mambo yako safi na hawataki kusikiaa sijui nini hakipo au ooh ngoja kwanza hizo habali wao hawataki,yaani wao wanataka kuishi kama queen Elizabert wa uingereza au Marie Antoniete ufaransa, Wanajifanya wamechoka pasipo kufanya kazi yoyote ile.mabinti wa kidigitali anawaza leo ataenda kula kwenye mgahawa gani na ataenda kula nn,hataki kusikia mambo ya kusonga ugali sijui kumenya ndizi hawataki wanataka kuona vitu vipo tayari wanataka maisha ya juu wakati wakati uwezo hakunaa na mda wote wanasubiri miujizaa..√√
Sasa ukikutana na binti wa namna hiyo kijana andaa pesa za kumpeleka kwenye migahawa,maana yake kama unapokea 800000 andaa 300000 ya kula kwenye migahawa na kwenye masupamaketi mjini,hapo utanunua msosi sana tu kijana,kijana najua unawapapalikia sana ukiwaona wameulamba wamependeza basi unaanza kuwatamani lakini jiandae pia maana mabinti wa kisasa hawapendi shida ndogo mdogo.
Yani hawama mabinti wa kisasa wanawaza kula kwenye migahawa na kwenye masupa maketi saa zote, tena usipokaza hata chai ataenda kununua.na usipofanya ivoo atakwambia ww humjali,atakwambia hujui kuhudumiaa ivoo bora muachane maana anaona anateseka tuu,yeye hataki kujua kama huna hela.hapa ndipo utamajibu kwa nn wanaume tunakufa mapema...√√
2. Usishangae nguo zako kutofuliwa wiki mbili au tatu,wao mda mwingi yupo anachatika tuu,yaani yeye kama ndio kuna masofa utakuta kanyoosha miguu juu kama sijui anataka kufanyw nini ...??ameshika kisimu chake, anaweza kumuita mdogo ake amsaidie kufua uku yeye amekiweka tu . Yeye anachart tu na siyo kwamba anachati na wewe hapana anachati na mashotizo..√√
Ukimwambie masuala ya kufua atakwambia kuna sehemu naenda mara moja embuu fufua kidogo narudi,katika vitu ambavyo hawapendi kufanya basi nj mambo ya kufuafua manguo,kijina nakushauli andaa kama 1mill au 2mill ukanunue mashine za kufulia au tafuta housegeli awe anakufulia lazivyo utaishia kuvaa nguo chafuu..√√
Kwanza utanunua nguo mpaka uchoke,kijana andaa kamaa 250000 kwa ajili ya nguo,maana kuna mabinti utafikiri wamezaliwa na nguo yeye kila akiona nguo mpyaa anataka avae,akimuona rafiki yake ana kitu kipya basi na yy anataka anunuliwee ..hapo nahisi unapata jibu kwa nn wanaume tunakufa mapema....√√
3. Kupiga deki sahau kijana mwenzangu. Aanze tu kupinda mgongo.yaani binti wa sasa aanze kupiga deki ataona amejishusha sana,yeye anachojua ni kwamba chumba Kama unataka usafi wa nyumba yako tafuta housegirl.kizazi cha sasaivii ni kigumu sanaa,ukioa mke mjini ni matatizo matupu,ukioa mke kijijini piaa ni kero tupu lazima uanze kumfundisha kwana namna ya kuishi na hiyo course itachukua miaka 3 na baada ya hapo ni matatizo juu ya maproblemu,kijana jiandae kutafuta mfanyakazi wa ndani zaidi ya hapo utainama mweyewe...√√
Usije ukashangaa akakwambia na wewe mara mojamoja uwe unadeki,kilaa siku mimi tu jamani,yaani anataka na ww udeki,au atakwambia hivi hauna mdogo wako kijijini aje tusaidiane kazi maana mwenyewe nachoka,kijana mabint wa kisasa hawa wapo kama kama kuku wa kisasa ukimgusa tu anakata moto....√√
4. Jua kuwa utawahi wewe kuamka, yeye bado kalala. Amechoka kazi za ofisini za jana yake.yaani hapo ndio majanga matupu,ukioaa msomi ndugu yangu jiandae kuwa wa kwanza kuamka,jiandae kuandaa chai,jiandae kufanya usafi ndani na njee,jiandae kupasi nguo maana yeye atakuwa amelala yaani amechoka na kulingana na kazi za maofisini.
na akiamkaa hapo atapitiliza kwenye smart foni yake na kuanza kuungalia page za udaku insta na twita bila kusahau facebook,au akiamka hapo anajiandaa kwenda kazini au akiamka cha kwanza ataulizia kama umepika chai,anaweza akamka akakwambia usiondoke kwanza naomba nioge unipeleke kazini lskini kabla hapo napitia mahali ndio unipeleke kazi,yaani mabinti wa kisasa wanaona kila kitu kipo sawa ..√√HAPO NAHISI UNAPATA JIBU KWA NINI WANAUME TUNAKUFA MAPEMA...√√
5. Bajet ya saloon na nguo iwepo ya kila wiki nywele na kucha.hapa ndipo patamu sana,yaani hawa mabinti wa kudigitali kila baaada ya wiki moja au siku 4 anataka kwenda salooni,hapo hapo atahitaji hela ya bodaboda au umpe usafiri wako au umpelekee huko anakotaka kwenda saloon,kamaa unapokea 800000 ujue 200000 itatumika kwa ajili ya saloon kwa nwezi hivyo kila baada ya miezi miwili itakuwa inakutoka 200000.
Yaani unaweza ukashangaa matumizi ni makubwa kuliko kipato jamani vijana jiandaeni mapema ila mkifikia huku msipate shida,twendeni tukalime mashamba ya mpunga na matikiti maji morogoro,na ukishindwa kuwahudumia atakwambia ulinioa kuja kuteseka uku..??atakwambia mm niliolewa na ww kwa bahati mbaya naomba nikamtafute mwenye mapenzi ya kweli,ukimpata mwanamke wa kidigitali kwanza ujue umeingia kwenye vita na pengine usipokuwa makini unaukaribisha umasikini√√
6.wao wanasema wanakwenda na wakati,,kijana ukirogwa ukaoa wanawake wa kidigitali basi hakutakuwa na mganga wa kukuponya,wanaboa kinoma hatari,mda atataka kila nguo inayopita macho mwake aipate wengi wanajiita mamodels,wanajiita madisigner masuala ya kuinamisha kiuno sijui kipika hawataki wanaogopa watakomaa mikono na ndio maana wengi vyakula wanapikiwa na mahousegal au wazazi wao.
hivyo basi kijana ukifanikiwa kuoa mke wa namna hii jipange na mda mwingi ni watu ambao wanakesha kamaa popo mchana wamelala usiku na mchana wanazunguka jiji zima utafikiri wanawanga,anaweza akaja siku moja akakwambia hivi mume kwenu babu yako hakukuachia hata kiwanja tuuze tununuee VEROSA maana nimechoka kutembea kwa miguu.nazani unapata jibu kwa nini tunakufa mapema....√√
Usilalamike xana ndio utu uzima huo,kuoa sio kwa kukimbiliaa hata siku moja ukiingia ujue umeingia kwnye ulimwengu mwingine kabisa raha kidogo shida sanaa ndio maana ya ndoa hiyoo,sasa kabla hujaingia ukoo jipange na uandae mazingira ya uhakika maana hakuna namna ndio wake zetu wa sasa wanapenda kuhudumiwa kuliko kuhudumiaa..
LAKINI USIACHE KUMUOMBA MUNGU AKUSAIDIE UPATE MWENYE HOFU YA MAISHA,UPATE ANAYEJITAMBUA NA KUJUA NINI ANAFANYA KWA WAKATI GANI....√√.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz