*MWANAMKE JUA MAMBO YANAYO HAMASISHA MAHABA KWA MUMEO* - EDUSPORTSTZ

Latest

*MWANAMKE JUA MAMBO YANAYO HAMASISHA MAHABA KWA MUMEO*

Image result for Jifunze jinsi ya kucheza na mwanamke mnene ndani ya sita kwa sita

(1) *KITANDA* 

_Mwanamke jitahidi kitanda chako kiwe vizuri NA cha kuvutui kipambe vizuri,kwa mashuka mazuri yenye nakshi,na shuka inyooke vizuri,sio kitanda kinakuwa kama vile stoo ya nguo chafu._ 

(2) *MANUKATO* 
_Katika chumba chako jitahidi sana,kiwe kinanuka kila Mara mumeo anapo rudi akiingiq chumbani akutane na harufu nzuri, .sio chumba chanuka jasho._

 (3) *USAFI* 

Hili ni jambo LA muhimu sana maana utakuta chumbani kuna vyupi vya wiki nzima, hazijafuliwa mataulo chini,masidiria,mumeo akikuta chumba kiko hivo ujue kuna shangingi atamchukua._ 

(4) *Usafi wa mwili* 

_PIa Usafi wa mwili mwanaume anavutiwa na utakavokuwa umejipamba na atavutiwa kimapenzi na wewe._

 (5) *Mapokezi mazuri*
 _Wanaume wanapendana sana kupokelewa vizuri,kwa mahaba tele mapokezi utakayo mpa mtu jitahidi yawe ya mahaba,legeza macho, mwili,yaani ili mradi tu umchanganye mwanaume Siyo umeshupaa kma mwanajeshi kwenye paredi._ 

(6) *CHAKULA* 
_Jitahidi mwanamke kujua kupika sio tu kupika michakula kama ya jela michukuchuku mibaya,mamchuzi chururu kama watoto wanapika matipwi._ 

(7) *MITEGO* 
_Hii ni njia ambayo watakiwa uwe mjanja ukimuona mumeo kakaa sebleni basi vaa hata shumizi jipitishe huku ukijitingisha Mara kwa Mara,ujue lazima atakutizama tu tena kwa mwendo nzuri wa maringo._ 

(8) *MAPENZI* 
_Mapenzi si lazima kitandani tu popote ni muhimu maana wengine mpaka mume amwambie cheza basi,kiuno kimekaza ukilala chamende ndo basi hata huyo mende anatikisa miguu loooh._

 (9) *UKARIMU NA KUJIPENDEKEZA* 

_Hata kama kwenu ulizoea kuwa na domo kama bakuli la togwa jitahidi kuchunga mdomo ukiona huwezi mumeo ngoja aondoke ufunge mlango ubwatuke peke yako kaa chizi,akirudi funga upuuzi wako zungumza maneno mazuri mnyenyekee._ 

(10) *MAKELELE* 

_WANAUME wengi huwa hawapendi makelele wanapenda wakirudi nyumbani kuwe kumetulia isiwe kma choo cha umma,WANAUME wanapenda ukimya mahala panapokuwa kimya huzidisha mapenzi._ 

(11) *ZAWADI* 
_Jitahidi kumnunulia vizawadi pindi unapokwenda sokoni au dukani mwanaume hujisikia faraja pale ukimpatia zawadi._ 

(12) *MAVAZI* 

_Pendelea kumchagulia mavazi TIZAMA rangi ya mwili wake kisha mchagulie nguo inayoendana na rangi yake ya mwili siyo mume mweusi waende kumvisha nguo nyekundu kma anaenda kupunga madogoli mamaa._ *MTUNZE MUMEO MAMA USIPOMTUNZA WAPO WATAKAO KUTUNZIA*




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz