DONGO NA MIKWARA YA SINGIDA UNITED KWA MBEYA CITY - EDUSPORTSTZ

Latest

DONGO NA MIKWARA YA SINGIDA UNITED KWA MBEYA CITY


Uongozi wa Klabu ya Singida United umefunguka na kuanza kujigamba kuwa utapambana kadri ya uwezo wao katika michuano ya ligi kuu ili historia yao iweze kubaki salama huku wakiwatitishia wapinzani wao Mbeya City kwamba wao sio ngazi ya kuwapandisha wengine daraja
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Singida United Festo Sanga ikiwa yamebakia masaa machache kuelekea mtanange wao dhidi ya Mbeya City leo Aprili 27, 2018 katika dimba la Sokoine mjini Mbeya katika muendelezo wa michezo ya ligi kuu Tanzania Bara.

"Tunaenda kucheza na Mbeya City tukiwa tunawaheshimu kwani wametoka sare na timu kubwa kama Yanga hivyo naamini hata sisi wametupania na pia wanahitaji kujiondoa katika nafasi waliyopo, lakini sisi sio ngazi ya wengine kung'ang'ania kutokushuka daraja. Sisi tunacheza mpira na hatuingii uwanjani kumpa mpinzani wetu pointi tatu bali tunapambana", amesema Sanga.

Pamoja na hayo, Sanga ameendelea kwa kusema "tunapambana kadri ya uwezo wetu ili kwenye Ligi kuu historia yetu iweze kubaki kuwa salama kwa maana tunahitaji kuwa kwenye nafasi ya nne, tatu au mbili na hilo linawezekana kwa sababu mpira unadunda na bado tuna mechi tano kabla ya kumaliza Ligi kwa hiyo hauwezi jua kitakachotokea".

Singida United inashuka dimbani ikiwa nafasi ya tano kwa alama 37 kwa michezo 25 kibindoni katika msimamo wa ligi kuu, Mbeya City akishika nafasi ya 10 kwa alama 26 yenyewe ikiwa na michezo 24 mpaka sasa waliyofanikiwa kuicheza.


NA ISMAEL MOHAMED EATV

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz