TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA LEO TAREHE 20 MARCH - EDUSPORTSTZ

Latest

TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA LEO TAREHE 20 MARCH

Mohammed Salah ananyatiwa na barcelona, Real Madrid na PSG

Barcelona, Paris St-Germain na Real Madrid zinataka kumsajili mshambuliaji wa Liverpool Mohammed Salah , 25 kwa dau la uhamisho litakalovunja rekodi la £200m. Raia huyo wa Misri amefunga mabao 28 katika ligi ya Uingereza msimu huu. (Sun)
Luke Shaw na Mourinho

Beki wa Manchester United Luke Shaw, 22, anahisi kwamba meneja Jose Mourinho anamnyanyasa na kwamba raia huyo wa Uingereza huenda akawasilisha malalamishi yake kwa naibu afisa mkuu mtendaji katika klabu hiyo Ed Woodward. (Mirror)
Mourinho anapanga kumsajili kiungo wa kati wa Arsenal na Wales Aaron Ramsey, 27, katika klabu ya Manchester United. (Star)

Beki wa kulia wa Arsenal Hector Bellerin

United tayari imemuulizia beki wa Arsenal Hector Bellerin, lakini Juventus wanapigiwa upatu kumsajili mchezaji huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 23. (Mirror)

Pendekezo la mshambuliaji wa Bosnia Edin Dzeko kuhamia Chelsea mwezi Januari liligonga mwamba baada ya Roma kujiondoa katika mkataba huo wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32.(Radio Rai, via Metro)

Mkufunzi wa klabu ya Bayern Munich Jupp Heynckes amepinga usajili wa mshambuliaji wa Bordeaux Malcom, 21. Raia huyo wa Brazilian amehusishwa na uhamisho wa Tottenham na Arsenal. (Evening Standard)

Mshambuliaji wa Liverpool Roberto Firmino anasema kuwa Liverpool ililazimika kubadilisha mtindo wa mchezo wake kufuatia uhaimsho wa mshambuliaji wa Brazil Philippe Coutinho aliyehamia Barcelona. (Goal)

Mwandishi wa New York Times Rory Smith anaamini Firmino ataipatia hamu Bayern Munich kumsajili iwapo mshambuliaji wa klabu hiyo raia wa Poland Robert Lewandowski, 29, ataondoka mwisho wa msimu huu . (BBC Radio 5 live)

Utafiti wa uhamisho unadai kwamba mshambuliaji wa Tottenham nchini Uingereza Harry Kane ataipatia faida kubwa Tottenham zaidi ya Lionel Messi kwa Barcelona.. (Express)

Beki wa Chelsea Andreas Christensen aliomba ushauri kwa nahodha wa zamani wa klabu hiyo John Terry - anayechezea Aston Villa - baada ya kiwango chake cha mchezo kudorora. (Eurosport Denmark, via Evening Standard)

Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi amefichua kwamba hatapiki tena wakati wa mechi kwa sababu hatumii tena chokoleti na vinywaji vyenye gesi. (Goal)

Mshambuliaji wa Ureno na Real Madrid Cristiano Ronaldo aliwahakikishia wenzake wa Real Madrid kwamba atashinda taji la mfungaji mwenye mabao mengi katika ligi ya La Liga licha ya Messi kuwa na mabao 11 zaidi ya yake. (Marca)

Brazil itatumia uwanja wa mazoezi wa Tottenham kuajiandaa katika kombe la dunia la Urusi mwisho mwa msimu huu. (Evening Standard).


EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz