ARSENAL APIGWA KICHAPO NA TOTTENHAM - EDUSPORTSTZ

Latest

ARSENAL APIGWA KICHAPO NA TOTTENHAM


Mshambuliaji wa Tottenham Hotspurs akifunga bao lililoipatia ushindi timu yake dhidi ya Arsenal


Mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane ndiye anayeshikilia hatma ya klabu hiyo kulingana na mkufunzi wa klabu hiyo Mauricio Pochettino, kufuatia mchezo wake uliosaidia timu hiyo kuwalaza maadui zao wa mjini London.

Kichwa kikali kilichopigwa na Kane kilimwacha kipa Petr Cech bila jibu na kutingisa wavu katika mechi hiyo ya debi ya London inayoiweka Hotspurs katika nafasi ya tatu katika jedwali la ligi.

Kane Aliruka juu ya beki wa Arsenal Laurent Kolscieny katika dakika ya 49 na kufunga krosi iliopigwa na Ben Davie .

Na ulindaji lango mzuri wa Cech ulioweza kuizuia Spurs katika kipindi cha pili, akipangua mashambulio kadhaa na hivyobasi kuiweka Arsenal katika mchuano huo.

Mchezo wa Tottenham iliotawala kila safu uliwawacha wachezaji wa Arsenal mdomo wazi huku mchezaji wa ziada Alexandre Lacazette akikosa nafasi mbili za wazi, mojawapo akiwa amesalia na kipa Hugo Lloris na kupiga nje.

Elimu Yetu
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz