MWADUI FC YAWAKALISHA KAA LA MOTO YANGA - EDUSPORTSTZ

Latest

MWADUI FC YAWAKALISHA KAA LA MOTO YANGA



NDG MSOMAJI WA EDUSPORTSTZ UNAKUMBUSHWA KUSUBSCRIBE NA KUFOLLOW WEB YETU PAMOJA NA MITANDAO YETU YA KIJAMII CHINI YA POSITI HII ILI KUTUMIWA UPDATES ZOTE ZA AJIRA, MICHEZO, HABARI, SCHOLARSHIPS PAMOJA NA MASTORI YA MASTAA NA VIONGOZI MBALIMBALI. EDUSPOTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI.
Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Yanga wamelazimishwa suluhu na Mwadui FC kwenye mchezo wa raundi ya 13 uliomalizika jioni hii uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Yanga chini ya kocha Mzambia George Lwandamina kwa mara ya kwanza tangu arudi kutoka kwao, imeshindwa kupata ushindi hivyo kubaki katika nafasi ya tano. Mwadui FC yenyewe imefikisha alama 13 na kupanda hadi nafasi ya 9.

Hii ni mechi ya pili Yanga inashindwa kupata ushindi ambapo mechi ya raundi ya 12 Disemba 2017, ilikubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Mbao FC ya Mwanza.

Yanga imefikisha alama 22 hivyo kushindwa kuifikia Mtibwa Sugar yenye alama 23 katika nafasi ya nne baada ya wikiendi iliyopita kushinda mechi yake ya raundi ya 13 dhidi ya Lipuli FC.

Kesho kutakuwa na michezo miwili ambapo vinara wa ligi Simba SC watakuwa wenyeji wa Singida United wakati Azam FC inayoshika nafasi ya pili itakuwa ugeneini mjini Ruvuma kucheza na Majimaji FC.EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati. BOFYA HAPA KUJIUNGA NA INNOVATION FURSA CHALLENGE http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
UNGANA NASI KUPITIA LIKI HIZI ILI KUTUMIWA HABARI POPOTE ULIPO


EDUSPORTSTZ NI FAHARI YA WASOMAJI

WEKA EMAIL YAKO:


Delivered by EDUSPOTSTZ
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno
EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz