MAJIBU YA MZEE AKILIMALI KWA WANACHAMA WA YANGA - EDUSPORTSTZ

Latest

MAJIBU YA MZEE AKILIMALI KWA WANACHAMA WA YANGA





Mwanachama wa siku nyingi wa klabu ya Yanga, Ibrahim Akilimali ameshangazwa na wale wanaotaka avuliwe uanachama na kusema hawana jeuri hiyo.

Pamoja na kuibuka na kusema hivyo, Akilimali amesema kama atafanyiwa figisu na kuondolewa Yanga, yeye na wazee wenzake watakwenda hadi ikulu ya Rais Magufuli na kufikisha malalamiko yao.

Leo mchana, baadhi ya wanachama wa Yanga walitaka Akilimali kuondolewa uanachama kwa kuwa amekuwa akizuia mabadiliko ya klabu hiyo.

"Nimezuia mabadiliko yapi, mimi ni kati ya wale tuliotaka mabadiliko hata wengine hawajawa wanachama.

"Tatizo hawa wenzetu wanataka mambo ya haraka na ili mradi kuwaridhisha watu. Lazima tufuate utaratibu na hii ni lazima.

"Kama wanataka kuigawa klabu wanajidanganya na mimi na wazee wenzangu kamwe hatuwezi kukubali," alisema.



EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz