KIUNGO WA ARDERNAL CARZOLA ASEMA NUSRA AKATWE MGUU WAKE - EDUSPORTSTZ

Latest

KIUNGO WA ARDERNAL CARZOLA ASEMA NUSRA AKATWE MGUU WAKE




KIUNGO wa Arsenal, Santi Cazorla, amesema ilibaki kidogo akatwe mguu wake baada ya kupata jeraha mguuni ambalo limemweka nje ya uwanja kwa muda mrefu sasa.

Cazorla amesema matatizo ya msuli mkubwa wa mguu, ndiyo yaliyosababisha madhara katika mguu wake kiasi cha kutakiwa kukatwa lakini daktari alipambana kutibu tatizo lake.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32, hakuichezea Arsenal tangu Oktoba, mwaka jana, huku tatizo lake likionekana kuwa sugu kwa miezi 11 japokuwa sasa nafuu imeanza kuonekana.

Cazorla alikumbana na tatizo hilo la kuumia msuli mkubwa wa mguu mara mbili, lakini mara hii ya pili ndiyo iliyoonekana kuwa na tatizo zaidi kwake kiasi cha kutishia kukatwa mguu wake kutokana na maambukizi.

Cazorla alisema: “Daktari aliniambia, kama sasa naweza kutembea na mtoto wangu katika bustani iliyo nyumbani kwangu, ni jambo la kushukuru sana.

“Maambukizi yalisambaa kidogo kiasi cha kutishia kukatwa kwa mguu wangu, lakini madaktari walipambana na tatizo mpaka sasa naendelea vizuri, hakikuwa kipindi kizuri kwangu.”

Ni kiasi cha kusubiri kutazama hali ya afya ya Cazorla, japokuwa mwenyewe amesema anatarajia kurejea uwanjani akiwa fiti Januari, mwakani.
like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika



Edusportstz


TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA







For Booking>>>







EMAIL: edusportstz@gmail.com












CALL>>>







Voda: +255757441463







JIUNGE NAMI KUPITIA LINK HIZI












INSTAGRAM
FACEBOOK







SUBSCRIBE YOUTUBE CHANEL
















DOWNLOAD EDUSPORTS ANDROID APPLICATION CLICK HERE










Follow @bakalemwatz


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz