BALE KUREJEA UWANJANI LEO - EDUSPORTSTZ

Latest

BALE KUREJEA UWANJANI LEO



Gareth Bale amekua akikumbwa na majeraha ya mara kwa mara

Mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale atacheza kwa mara ya kwanza siku ya Jumanne baada ya kukaa nje kwa miezi miwili.

Kocha wa Madrid Zinedine Zidane amesema Bale tiyari amepona na kwa sasa yupo tiyari kurejea uwanjani kuongeza nguvu katika kikosi chake ambacho hakionekani kufanya vizuri kama misimu miwili iliyopita.

Bale amekuwa nje kutokana na kupatwa na majereha ya goti na baadae nyonga na kwa sasa amejumuishwa katika timu itakayocheza na Fuenlebrada kwenye kombe la Copa del Rey.

Bale raia wa Wales alionekana mara ya mwisho uwanjani walipoichapa Borussia Dortmund 3-1 kwenye kombe la klabu bingwa Ulaya.

Bale ambaye pia alikosa kucheza wakati timu yake ya Wales ikisaka kufuzu kombe la dunia, hajacheza sambamba na Cristiano Ronaldo ama Karim Benzema tokea kuanza kwa msimu huu kwa sababu ya majereha ama kuwa na adhabu.
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati http://www.edusportstz.com ni fahari ya wasomaji
Follow web yetu na like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika,ni rahisi mno


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz