OMOG APEWA NAFASI NYINGINE - EDUSPORTSTZ

Latest

OMOG APEWA NAFASI NYINGINE




Simba inataka kumpa mikoba Joseph Omog - Goal.com


Pamoja na taarifa kuendelea kuzagaa kwamba Kocha Joseph Omog kiota kimeanguka,

Kamati ya Utendaji ya Simba imekutana na kukubaliana Kocha Joseph Omog kuendelea kukinoa kikosi hicho.


Omog amekuwa katika hali ya hatihati kama vile atafukuzwa kazi kutokana na mwenendo wa timu yake.


Lakini taarifa kutoka ndani ya Simba zinaeleza, katika kikao hicho wamekubaliana Omog kuendelea na kazi yake.


“Lakini ametakiwa kubadili mambo na kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, Simba inataka ushindi,” kilieleza chanzo.


Mwenendo wa Simba katika mechi nane ilizocheza imekuwa ni milima na mabonde kwa kupitia ushindi, sare, ushindi sare.


Hali hiyo imesababisha kuwepo kwa taarifa nyingi ambazo zinaeleza kwamba Omog anakaribia kutimuliwa.



Hata hivyo, bado hali inaonekana kuwa haijatulia na Omog atalazimika kufanya kazi ya ziada kuhakikisha anabadili mambo.

 like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika Propellerads

For Booking>>>



CALL>>>

Voda: +255757441463

JIUNGE NAMI KUPITIA LINK HIZI










Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz