WAYNE ROONEY ATIWA MIKONONI MWA POLISI - EDUSPORTSTZ

Latest

WAYNE ROONEY ATIWA MIKONONI MWA POLISI




Wayne Rooney.

Mshambuliaji wa Everton Wayne Rooney amekamatwa na baadae kuachiliwa kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa, polisi mjini Cheshire imesema.

Rooney alikamatwa baada ya polisi kusimamisha gari aina ya Volkswagen Beetle ambayo alikuwa anaendesha. Polisi wa Cheshire wanasema Rooney mwenye miaka 31, ana mashtaka ya kujibu kwa kukutwa akiendesha gari akiwa amelewa na akiwa pia kwenye mwendo mkali.

Nahodha huyo wa zamani wa England na Manchester United ameachiliwa, lakini kesi yake itasikilizwa baadae mwezi huu. Rooney ambaye amestaafu soka la kimataifa mwezi uliopita, ndiye anashikilia rekodi ya ufungaji mabao muda wote kwenye timu ya taifa akiwa na magoli 53.

Alijiunga tena na klabu yake ya utotoni Everton, miaka 13 baada ya kuondoka Merseyside kwenda Manchester United.


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz