KAPOMBE SASA FITI KUANZA MAZOEZI KUTOKANA NA MAUMIVU YA NYONGA - EDUSPORTSTZ

Latest

KAPOMBE SASA FITI KUANZA MAZOEZI KUTOKANA NA MAUMIVU YA NYONGA






Hali ya beki wa kulia wa Simba, Shomari Kapombe inaonekana kumridhisha daktari wa timu hiyo na sasa amempangia kuanza mazoezi Jumatatu ijayo.


Kapombe ataanza mazoezi Jumatatu baada ya zile wiki mbili za nyongeza kwisha.


Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema kuwa mazoezi ya Kapombe yatakuwa ya taratibu.


"Ataanza mazoezi taratibu kwa kuwa ndiyo anarejea katika mazoezi," alisema.


Kapombe amekuwa akisumbuliwa na nyonga, jambo ambalo Simba waliamua kulifanyia kazi kwa kina kuhakikisha anakuwa katika hali yake.


Beki huyo amerejea Simba ambayo aliondoka na kwenda kujiunga na Azam FC kabla ya kwenda nchini Ufaransa ambako alijiunga na AS Cannes, hata hivyo, hakudumu sana.


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz