ZLATAN IBRAHIMOVIC KUREJEA MANCHESTER UNITED - EDUSPORTSTZ

Latest

ZLATAN IBRAHIMOVIC KUREJEA MANCHESTER UNITED

 Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic (Kulia).KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho amefunguka kuwa mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic anaweza kusaini mkataba na timu hiyo. Msimu uliopita mshambuliaji huyo alifanya vizuri na kikosi cha United lakini baada ya mkataba wake kumalizika mwishoni mwa msimu hakuongezewa mwingine kutokana na kutarajiwa kukaa nje hadi mwakani kutokana na kukumbwa na majeraha ya goti.Kwa sasa United wanatarajiwa kumsimamisha mshambuliaji Romelu Lukaku, kama mshambuliaji wao wa mwisho baada ya kumsajili hivi karibuni akitokea Everton.“Tumetumia fedha nyingi kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji kwa kuwa nafasi hiyo ina vitu viwili, aidha upate mshambuliaji utumie fedha au usimpate. “Lakini pia tumefanya hivyo kwa kuwa tunajua kuwa tutamkosa Zlatan kwa miezi sita ya mwanzoni mwa ligi,” alisema Mourinho. Hii ina maana kuwa Zlatan ambaye msimu uliopita alifanikiwa kuifungia timu hiyo mabao 28, ataisaini mkataba mwingine wa kuitumikia United kwa msimu ujao.

Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic (Kulia).

KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho amefunguka kuwa mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic anaweza kusaini mkataba na timu hiyo. Msimu uliopita mshambuliaji huyo alifanya vizuri na kikosi cha United lakini baada ya mkataba wake kumalizika mwishoni mwa msimu hakuongezewa mwingine kutokana na kutarajiwa kukaa nje hadi mwakani kutokana na kukumbwa na majeraha ya goti.

Kwa sasa United wanatarajiwa kumsimamisha mshambuliaji Romelu Lukaku, kama mshambuliaji wao wa mwisho baada ya kumsajili hivi karibuni akitokea Everton.

“Tumetumia fedha nyingi kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji kwa kuwa nafasi hiyo ina vitu viwili, aidha upate mshambuliaji utumie fedha au usimpate.



“Lakini pia tumefanya hivyo kwa kuwa tunajua kuwa tutamkosa Zlatan kwa miezi sita ya mwanzoni mwa ligi,” alisema Mourinho. Hii ina maana kuwa Zlatan ambaye msimu uliopita alifanikiwa kuifungia timu hiyo mabao 28, ataisaini mkataba mwingine wa kuitumikia United kwa msimu ujao.


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz