Panucci apewa kazi ya kuinoa Albania - EDUSPORTSTZ

Latest

Panucci apewa kazi ya kuinoa Albania


Christiani Panucci
Chama cha soka cha nchini Albania (AfA) kimemteua beki wa zamani wa timu ya taifa ya Italia Christian Panucci kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya nchi hiyo.
Panucci anachukua mikoba ya kocha wa zamani wa taifa hilo Gianni De Biasi,ambae alijiuzulu mwezi uliopita.

Raisi wa chama hicho cha soka Armand Duka amesema kazi ya kwanza ya kocha huyo mpya ni kufuzu kwa fainali za michuano ya ulaya ya 2020.

Panucci aliwahi kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Urusi chini ya Fabio Capell, pia amewahi kuvifundisha vilabu vya Livorno na Ternana vya Seria B.na amewahi kuvichezea vilabu vya Real Madrid na As Roma,


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz