Marco Silva ajiuzulu umeneja Hull City - EDUSPORTSTZ

Latest

Marco Silva ajiuzulu umeneja Hull City




Marco Silva meneja wa Hull City amejiuzulu kuendelea kuinoa timu hiyo iliyoshuka daraja kutoka ligi kuu ya nchini England.
Silva mwenye miaka 30 raia wa Ureno alichukua mikoba ya timu hiyo toka kwa Mike Phelan mwezi Januari na jukumu lake lilikuwa ni kuisaidia timu hiyo isishuke daraja.

Meneja huyo wa zamani wa Sporting Lisbon na Olympiakos anahusishwa na mpango wa kwenda kujiunga na timu ya Watford ambayo imemtimua mkufunzi wake wa kiitaliano Walter Mazzarri.

Mbali na Silva makocha wengine pia wamejiondoa kwenye timu hiyo ambao ni kocha msaidizi Joao Pedro Sousa,kocha wa kikosi cha kwanza Goncalo Pedro pamoja na kocha wa makipa Hugo Oliveira


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz