Wachezaji wa Yanga wanatarajia kuondoka leo usiku nchini Algeria kurejea nyumbani.
Sasa wanatarajia kuondoka na ndege ya Emirates badala ya Turkish Airways
na imeelezwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limelazimika kutoa
mkopo kwa klabu hiyo ili kuwakomboa.
Wachezaji saba na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa
walichelewa ndege jijini Algeria na kulazimika kusubiri hadi Jumanne
kesho ndiyo waondoke na kutua nchini kesho.
Mkwasa alisema wataomba msaada kwa MC Alger waliokwenda kucheza nao na kufungwa mabao 4-0 kwa kuwa hawakuwa na fedha za kutosha.
No comments:
Post a Comment