Kikosi cha Simba kimehitimisha pre-season nchini Misri ambapo leo timu inatarajiwa kurejea nchini kuhitimisha awamu ya mwisho ya maandalizi
Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amepata takribani wiki nne kukiandaa kikosi chake kambi ikianzia mji wa Ismailia na kisha kuhitimishwa Cairo
Sehemu kubwa ya wachezaji wamepata wa kutosha wa maandalizi ukiondoa wachezaji wachache ambao walichelewa kutokana na changamoto za vibali huku kiungo Neo Maema akitua baada ya kumaliza majukumu ya kuitumikia timu ya Taifa ya Afrika Kusini kwenye michuano ya CHAN 2024
Baada ya kurejea nchini Simba itakuwa na wiki moja zaidi ya kujiandaa kabla ya Tamasha la Simba Day litakalofanyika Septemba 10
Mnyama atakuwa siku nyingine chache za kujiandaa kabla ya mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ambao mpaka sasa ratiba inaonyesha utapigwa Septemba 16
Baadae Simba itaelekea Botswana kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Gaborone United utakaopigwa Septemba 20
Usikose kutazama mechi zote za LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA, MASHINDANO YA CAF LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA au HAPA kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.
.jpeg)
Post a Comment