Laana Duniani.... Watoto Wamuua Baba Yao Kisha Watupa Mwili Wake Kisimani - EDUSPORTSTZ

Latest

Laana Duniani.... Watoto Wamuua Baba Yao Kisha Watupa Mwili Wake Kisimani




Katika hali ya kushangaza huko nchini Kenya Watoto wawili wamemuua baba yao huku chanzo cha mgogoro kinatajwa kuwa ni kugombea mali za urithi.


Kwa mujibu wa taarifa kutoka nchini humo zimebainisha kuwa Ndugu hao wawili wanaripotiwa kumshambulia baba yao kabla ya kumuua na kuutupa mwili wake ambao hauna uhai ndani ya kisima ndani ya eneo hilo.


Kufuatia kutekeleza mauaji hayo Jeshi la Polisi huko Kisii limewakamata ndugu wawili wanaoaminika kumuua baba yao kufuatia kutokubaliana juu ya urithi wa mali za huyo kwa wanawe.


Dada yao na mjomba wao waligundua mwili wa mtu huyo baada ya kuona kitu sio sawa mtoni. Walimkuta ndani kabisa ya kisima na mkono wake umefungwa, ukikatwa na panga na baadhi ya mbavu kuvunjika.


Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi nchini humo,umebainisha kuwa Matokeo ya kifo cha marehemu yalifichua kwamba alikuwa na jeraha kubwa ndani ya kichwa chake linalofanana na nyundo na alikuwa na urefu wa inchi nne kama ilivyothibitishwa na binti ya marehemu.




Familia sasa inadai haki wakati uchunguzi unapoanza kukusanya ushahidi wa kutosha kuwashtaki washukiwa. Watoto wamehimizwa kuwaheshimu wazazi wao haswa wakati na juhudi wanayoweka ili kuwalea.


Kutokana na tukio hilo la Baba kuuawa Na Wanawe Wawili huko Kisii tukio hilo limezua huzuni miongoni mwa Wananchi ambao wamewataka watoto kujibidisha katika kufanya kazi na kuacha kutegemea mali za urithi.



Watoto wavivu ndio asilimia kubwa huwaza kuhusu mali za urithi za wazazi,Ni jukumu la Wazazi kufundisha watoto kujituma katika kufanya ili waweze kujipatia maendeleo katika jamii kwa sababu kazi ni kipimo cha maendeleo.


Katika hatua nyingine,Matukio ya Vijana kufanya mauaji yamekithiri katika jamii kutokana na vijana kukosa maadili katika jamii.Hivyo basi elimua ya maadili miongoni mwa wazazi yafaa iendelee kutolewa kwa maana ya kuwafanya vijana kuwaheshimu wazazi na kupenda kufanya kazi.

Tazama ROSA REE Akiteswa na SHETANI Hapa Chini:






Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz