MCHEZAJI AFARIKI KWA KUGONGANA UWANJANI - EDUSPORTSTZ

Latest

MCHEZAJI AFARIKI KWA KUGONGANA UWANJANI


Huda ametajwa na klabu yake kama shujaa halisi

Mlinda mlango wa klabu ya ligi kuu ya Indonesia amefariki baada ya kugongana na mchezaji mwenzake uwanjani.

Choirul Huda, mwenye miaka 38, alikimbizwa hospitalini siku ya Jumapili lakini muda mfupi baadae ilitangazwa kwamba amefariki dunia.

Katika taarifa iliyotolewa na tovuti ya klabu yake Persela FC , daktari wa timu Yudistiro Andri Nugroho amesema mchezaji huyo alifariki baada ya kupata madhara makubwa kifuani.

Anasema mgongano huo ulisababisha kushindwa kupumua kwa Huda.Mashabiki wakiomboleza kifo chake

Ameongeza kuwa madaktari walijaribu kuokoa maisha yake bila mafanikio.

Mchezo huo uliisha kwa Persela kuifunga Semen Padang 2-0.

Maelfu ya mashabiki wamefika hospitalini alipofia mchezaji huyo aliyecheza michezo 500 ya ligi kuu kwa klabu yake pekee.
like facebook page yetu hapa kwa habari za uhakika Propellerads

For Booking>>>



CALL>>>

Voda: +255757441463

JIUNGE NAMI KUPITIA LINK HIZI










Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz