Kuna 'surprise' usajili wa Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

Kuna 'surprise' usajili wa Yanga

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Vyombo mbalimbali vya habari nchini Uganda vimeripoti taarifa ya beki kisiki wa SC Villa Gift Fred kusajiliwa na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga


Fred alikuwa nahodha wa SC Villa ambapo katika msimu uliopita alishinda tuzo ya beki bora wa msimu


Beki huyo pia amekuwa sehemu ya kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda inayonolewa na Kocha Micho. Pia anamudu kucheza nafasi ya kiungo mkabaji


Beki kapanda hewani (wa kwanza kushoto pichani chini), mwili jumba! mwamba haswa katika kucheza mipira ya juu!


Taarifa za ndani zimebainisha kuwa Yanga imemsajili Fred kuchukua nafasi ya Mamadou Doumbia ambaye tangu aliposajiliwa kwenye dirisha dogo msimu uliopita, hakuweza kujihakikishia nafasi kwenye kikosi cha kwanza


Huu unaweza kuwa usajili wa 'surprise' kwani tayari Yanga ilishatangaza kukamilisha usajili wake


Wananchi wanasubiri utambulisho wa wachezaji wao wapya ambapo Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema wakati wowote wanaanza kushusha 'vyuma'



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz