Wekundu wa Msimbazi Simba Sc wako mkoani Mtwara ambapo jioni ya leo watashuka uwanja wa Nangwanda Sijaona kuikabili Azam Fc katika mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC)
Mechi muhimu kwa Simba kuisaka fainali katika michuano pekee ambayo inaweza kuipa Simba taji msimu huu
Hautakuwa mchezo mwepesi kwani ni derby inayozikutanisha timu ambazo zina nafasi sawa katika kuhitimisha msimu huu
Kama ilivyo kwa Simba, Azam Fc wamefanya uwekezaji mkubwa wa kikosi chao hata hivyo uwekezaji huo haukuwapa mafanikio waliyotarajia
Matumaini pakee waliyonayo ni kutwaa taji la FA, kwao hii inaweza kuwa mechi kubwa zaidi msimu huu
Kwa misimu ya karibuni Azam Fc wamekuwa wagumu kila wanapokutana na Simba. Katika mechi mbili za Ligi Kuu, Azam Fc walishinda mchezo mmoja na kulazimisha sare katika mchezo mwingine
Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana katika michuano ya FA, Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 ukiwa ni mchezo wa nusu fainali mwaka 2021
Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira aliweka nguvu kubwa katika mchezo huu, akiwapa mapumziko nyota wake muhimu katika mchezo wa ligi kuu uliopita dhidi ya Namungo
Ni mazingira hayo yanayoufanya mchezo huu kuwa muhimu kwa Robertinho na benchi lake la ufundi, kwani kama matokeo yatakuwa tofauti na ushindi, watatishwa mzigo wa lawama kwa maamuzi waliyofanya kwenye mchezo dhidi ya Namungo
Sare dhidi ya Namungo Fc ni kama iliiondoa Simba kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu na sasa matumaini yamebaki kwenye FA
Wanasimba hawawezi kujivunia chochote msimu huu kama timu yao haitatwaa taji la FAMechi itakuwa LIVE kwenye app yetu bofya hapa kuidownload ili usipitwe na mechi hii na nyingine nyingi
No comments:
Post a Comment