JINSI YA KUTUMIA MLONGE KWA MATOKEO YA AFYA BORA NA IMARA* - EDUSPORTSTZ

Latest

JINSI YA KUTUMIA MLONGE KWA MATOKEO YA AFYA BORA NA IMARA*

Close up portrait of a laughing african american man posing against white background Stock Photo - 45866044
DARASA LA MAHUSIANO
*MLONGE* ni moja kati ya mimea muhimu saana katika historia ya mwanadamu tangu kugundulika kwa mmea huu huko Asia miaka mingi iliyopita. Asili ya mti huu ni Uhindi ( India). Zipo nadharia zinazodai kuwa Mlonge kwa mara ya kwanza uligundulika huko India na wanasayansi wa Uingereza miaka mingi iliyopita tangu waingereza walipokuwa wanaitawala India, ambapo wahindi walikuwa wakitumia mmea huu kujitibu na kujikinga na mambo mbalimbali bila kufahamu umuhimu mkubwa zaidi juu ya mmea huu. Baadae ikaja kugundulika pia katika ukanda wa Afrika Magharibi kuna mimea hii kwa wingi saana hasa katika nchi ya Nigeria.
Mwishoni mwa karne ya 20 na mwanzoni mwa karne ya 21 Afrika mashariki ilionekana kuwepo kwa mimea hii kwa wingi hasa katika nchi ya Tanzania lakini watu wake hawajui umuhimu wa mmea huu. Mikoa kama Tanga, morogoro, kagera, Tabora, kigoma, Dodoma, lindi, mtwara, Rukwa na mikoa ya ukanda wa Joto na maziwa makuu imejaaliwa kwa wingi kuwa na miti hii ya Mlonge.
Mlonge hutumika kulisha mifugo, chakula cha watu ( mboga), kuboresha mashamba, kusafisha maji ya kunywa na hata mitishamba. Mlonge pia umegundulika kuwa ndio mti wenye maajabu zaidi duniani, mti huu una uwezo wa kutibu magonjwa zaidi ya 300 mwilini lakini kubwa zaidi Mlonge ni mmea lishe hivo hutumika kama kinga dhidi ya magonjwa.
*MLONGE UNA:*
1. Calcium mara 17 zaidi ya maziwa ya ng'ombe.
2. Una vitamini C mara 7 zaidi ya chungwa.
3. Potassium mara 15 zaidi ya ile ilioko kwenye ndizi.
4. Vitamini A mara 10 zaidi ya karoti.
5. Una protini mara 9 zaidi ya mtindi.
6. Una chrolophily mara 4 zaidi ya ile ya kwenye nyasi/ majani ya ngano ( wheatgrass).
7. Una madini chuma ( Iron) mara 25 zaidi ya spinachi
8. Una vitamini A-Z
9. Una amino acid muhimu zinazohitajika mwilini.
10. Una kiasi cha kutosha madini ya zinc ambayo ni madini muhimu katika kuongeza homoni za kiume, hamu ya tendo na nguvu kwa ujumla.
*MBEGU ZA MLONGE.*
Mbegu za Mlonge hutumika kama kiuaji sumu na pia hutibu uvimbe. Pia hutibu maumivu ya kwenye mishipa, gauti, kukakamaa kwa mishipa, magonjwa ya ngono, majipu pamoja na malaria sugu.
*MATUMIZI YA MBEGU ZA MLONGE.*
-Unaweza kuzitafuna kati ya punje 3 hadi 10 kwa siku.
- Unaweza kuzitwanga ama kuzisaga kupata unga wake.....
● Tumia unga wa mbegu za Mlonge kwenye chai,uji, maji moto ama kulamba.
●Kwa mtu mwenye presha, Uzito na mafuta mengi mwilini basi tafuna punje zake 2 kila baada ya masaa 2 au 3 na kunywa maji mengi.
*MAJANI YA MLONGE.*
Ikumbukwe kuwa kila kitu katika mmea wa Mlonge kinatumika na kina faida zinazofanana ( majani, mbegu, magamba na mizizi) lakini wengi hupenda kutumia majani ya Mlonge kwa sababu ni rahisi kuandaa lkin pia majani hayana ladha mbaya yaani hayana uchachu, uchungu wala ukali.
Unaweza kupika majani ya mlonge kama mboga ukala, pia unaweza kusaga majani baada ya kukausha vizuri kivulini na kupata unga wake.
*FAIDA ZA UNGA WA MAJANI YA MLONGE.*
1. Huondoa sumu mwilini.
2. Huboresha kinga ya mwili.
3. Husaidia mapambano dhidi ya kisukari.
4. Kupunguza uzito.
5. Huondoa makunyanzi usoni (Ant aging)
6. Huboresha macho na ubongo.
7. Hutibu vidonda vya tumbo.
8. Hutibu matatizo karibu yote ya ngozi.
9. Huongeza maziwa kwa wingi kwa Mama anaenyonyesha.
10. Hulinda Ini na figo.
11. Huongeza uwingi wa mbegu za kiume, hamu na nguvu kwa ujumla.
12. Hutibu U.T.I sugu na matatizo mengine kwenye mfumo wa kibofu cha mkojo.
13. Huongeza nguvu, umakini, ngozi yenye kupendeza na kutozeeka mapema.
14. Hutibu matatizo na maumivu ya mishipa.
15. Hutuliza mapigo ya juu ya moyo.
16. Hutuliza wasiwasi.
17. Hutuliza maumivu ya kichwa.
18. Huzuia na kushusha lehemu.
19. Hupunguza mafuta tumboni.
20. Husafisha kibofu.
21. Hurekebisha matatizo kwenye tezi.
22. Huondoa uchovu na kuchoka.
23. Husafisha damu.
24. Huondoa taka na makohozi mazito kifuani.
25. Hutibu homa na maumivu kwenye maungio.
26. Huondoa na kutibu minyoo sugu.
27. Hutibu malaria sugu.
28. Husaidia kujenga na kuimarisha misuli.
29. Hutibu TYPHORD sug




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz