Taarifa mpya kuhusu mechi ya Yanga vs Simba leo - EDUSPORTSTZ

Latest

Taarifa mpya kuhusu mechi ya Yanga vs Simba leo

ILE Siku ambayo ilikuwa ikisubiriwa ni leo Yanga vs Simba bado unajiuliza utaiangalia vipi mechi hii live buree bonyeza hapa kudownload app itakayorusha mechi hii live buree kabisa

Wananchiiiiii...! Ile siku imewadia.. Wanasema usiku wa deni haukawii kucha! Ni pale uwanja wa Benjamin Mkapa mtanange wa watani wa jadi kati ya Yanga dhidi ya Simba utapigwa

Ni Wazee Derby, Yanga ikiutumia mchezo huu kuwapa heshima Wazee ambao walitimiza vyema wajibu wao na kuhakikisha wanarithisha kizazi cha leo Yanga iliyo imara

Baada ya ushindi wa mabao 5-1 katika mchezo wa duru ya kwanza, matumaini ya mashabiki wa Yanga ni kuona timu yao ikiendeleza ubabe dhidi ya watani zao

Kama Yanga itashinda leo basi itajiweka katika nafasi nzuri zaidi katika mbio za ubingwa kwani wataongeza gap la alama dhidi ya washindani wake Azam Fc na Simba

Ni derby, itakuwa mechi ngumu ambayo itahitaji wachezaji kuvuja jasho jingi kuweza kupata matokeo mazuri

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesisitiza hawaendeshwi na fikra za ushindi mnono mara ya mwisho walipokutana na Simba

Wanafahamu huu utakuwa mchezo mpya ambao hata wapinzani wao watakuja kivingine kujaribu kulipa kisasi ingawa amewatahadharisha kisasi hicho kinaweza kuwatokea puani

Yanga inaelekea katika mchezo huu ikiwa na kikosi kamili. Wachezaji wote wa Yanga wako tayari kwa mchezo huu ni jukumu la Gamondi na benchi lake la ufundi kuamua silaha 11 atakazozitumia leo

Mageti ya uwanja wa Benjamin Mkapa yanatarajiwa kuwa wazi kuanzia saa 5 asubuhi



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz