UCHAMBUZI KUELEKEA MECHI YA MANCHESTER VS LIVERPOOL - EDUSPORTSTZ

Latest

UCHAMBUZI KUELEKEA MECHI YA MANCHESTER VS LIVERPOOL





Ligi Kuu England inaendelea tena Jumamosi ya leo kwa mechi kadhaa kupigwa, ambapo mechi inayosubiriwa kwa hamu ni ya Manchester United ambao wataikaribisha Liverpool pale Old Trafford.



Manchester United inaingia kucheza mchezo huu ikiwa na tofauti ya alama mbili mbele, dhidi ya Liverpool katika msimamo wa ligi.


Mpaka sasa Manchester ina ponti 62, na Liverpool ina 60 huku timu zote zinaingia kucheza mechi hii zikiwa zimecheza michezo sawa, michezo 21 ya ligi msimu huu.


Kuelekea mchezo huu, United inaikaribisha Liverpool Old Trafford ikiwa na rekodi mbaya ya kufungwa mechi 5 za ligi msimu huu, tofauti na Liverpool iliyopoteza 3 pekee.


Manchester imefunga jumla ya mabao 56 katika ligi, huku Liverpool ikiwa na zaidi ya United kwa kufunga mabao 67, hapo tunaona tofauti ni mabao 11.


Marouane Fellain anaweza akacheza mechi kuelekea kupona majera yake ya goti yaliyokuwa yanamsumbua, hali iliyosababisha kukosekana kwenye baadhi ya michezo ya ligi na hata UEFA Champions League.


Antonial Martial ana uwezekano wa kukosekana pia kwenye mchezo wa leo, huku Zlatan Ibrahimovic naye hatokuwepo sababu ya kusumbuliwa na goti pia.


Ander Herrera naye atakosekana kufutia majeraha ya nyama za paja, pamoja na Daley Blind ambaye pia ni majeruhi.


Liverpool wao wanaweza kuwa na Andrew Robertson, Jordan Henderson na Georginio Wijnaldum ambao hali zao kiafya zipo sawa baada ya kutoka majeruhini.


Mechi hii itaanza saa 9 na nusu kwa saa za Afrika Mashariki
EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz