DAKIKA 90 ZILIZOIPELEKA YANGA 8 BORA ASFC - EDUSPORTSTZ

Latest

DAKIKA 90 ZILIZOIPELEKA YANGA 8 BORA ASFC



Image result for YANGA

5' Buswita anachezewa faulo, mpira unapigwa kuelekea lango la Majimaji


6' Hassan Kessy anachezewa mazambi, na faulo inachezwa tena kuelekea Majimaji FC

9' Ibrahim Ajibu anafanya kazi safi kwa kupiga krosi langoni mwa Majimaji lakini mabeki wanaokoa

10' Mpaka sasa matokeo ni 0-0

13' Faulo inapigwa tena kuelekea Majimaji baada ya faulo

14' Kona inapigwa kuelekea Yanga, inapigwa lakini mabeki wanaokoa

14' Majimaji wanafanya shambulio lakini umahiri wa Youthe Rostand anadaka mpira


15' Bonaventure analisakama lango la Yanga lakini mwamuzi wa pembeni anasema ni offside

19' Faulo inapihwa na Ajibu kuelekea Majimaji, kushoto wa Uwanja, anapiga lakini kipa anaipangua na kuwa kona

21' Kona imepigwa lakini mabeki wa Yanga wanaibabatiza na kuwa goal kick

21' Bonaventure anachezewa faulo na mpira unapigwa kuelekea lango la Yanga

24' Mwinyi Haji anautoa mpira na unarushwa kuelekea lango la Yanga

24' Hassan anaupiga kichwa mpira uliopigwa na Peter Mapunda na kwenda nje, kona inapigwa lakini mabeki wa Yanga wanaokoa

26' Hatarii katika lango la Majimaji inatokea piga nikupige lakini mlinda mlango wa Majimaji anaokoa

27' Bonaventure anapiga shuti hafifu lakini linakuwa rahisi kwa Rostand kulidaka

28' Goli Kiki, mpira unapigwa kuelekea lango la Yanga, matokeo bado ni 0-0

29' Mwinyi Haji anapiga krosi kushoto mwa uwanja lakini mabeki wa Majimaji wanaokoa

31' Hassan Kessy anapiga free kiki lakini inaondolewa langoni mwa Majimaji na mabeki kwa kichwa

32' Goli kiki upande wa Yanga

33' Mapunda anapata nafasi ya kufunga lakini Mwamuzi wa pembeni anasema ni offside

34' Hatarii katika lango la Yanga baada ya Mapunda kubabatizana na Rostand na kupelekea kushindwa kufunga bao la kwanza

36' Pato Ngonyani anapewa kadi ya njano baada ya kucheza mazambi

38' Said Makapu anaubabatiza mpira na unatoka, sasa ni kona kwa Majimaji

39' Marcel anapiga kona mbovu ambayo inaokolewa na beki ya Yanga

40' Gooooli, Pius Biswita anafunga goli la kuongoza kwa njia ya kichwa baada ya krosi safi ya Mwinyi haji na kuweka bao la kwanza kwa Yanga. sasa Yanga ni 1 na Majimaji ni 0.

43' Haji Mwinyi anapiga krosi safi kuelekea lango la Majimaji lakini Yanga wanaokoa, zimesalia dakika 2 mpira uwe mapumziko.

45+' Dakika 3 zimeongezwa mpira uwe mapumziko, matokeo ni 0-1

45+ Mpira unarushwa kuelekea lango la Yanga baada ya wachezaji wa Majimaji kuutoa nje

Dakika 45 zimemalizika, Yanga wanaenda kifua mbele kwa bao 1-0 likifungwa na Buswita

49' Yanga wanapata kona ya kwanza kipindi cha pili kuafuatia golikipa wa Majimaji kuutoa mpira nje ulipogwa na Ajib

51' Offside langoni mwa Yanga baada ya mwamuzi wa pembeni kuumnyoshea kibendera Mapunda aliyekuwa anashambulia

57' Gooli, Emmanuel Martin anaifungia Yanga bao la kwanza kwa njia ya kichwa, sasa Yanga wako mbele kwa bao 2-0

61' Gooli, jafar Mohammed anaipatia Majimaji bao la kwanza

69' Mpira unarushwa kuelekea lango la Majimaji, sasa umetoka na unalekezwa tena lango la Yanga, matokeo ni 1-2

71' Yanga wanafanya mabidiliko, anatoka Rafael Daud na nafasi yake inachukuliwa na Yusuph Mhilu

72' Inapigwa kona kuelekea lango la Yanga lakini kipa Rostand anadaka mpira

72' Nahodha wa Majimaji, Hassan Hamis anapewa kadi ya njano baada ya kumfanyia mazambi Yusuph Mhilu, sasa ni free kick inapigwa na Ajibu

73' Faulo inapigwa lakini inaokolewa

76' Mpira umesimama kidogo baada ya wachezaji wa Majimaji kugongana

77' Zimesalia dakika 13 mchezo kumalizika

80' Peter Mapunda anaotea tena, Majimaji wanajitahidi kushambulia lango la Yanga wakitafuta bao la kuswazisha

81' Dakika 9 zimesalia, matokeo bado ni 2-1, Yanga wanaongoza

83' Hassan Kessy anapewa kadi ya njano, sasa ni faulo inapigwa kuelekea lango la Yanga.

84' Imepigwa lakini inakwenda nje

84' Paul Lyungu anaingia kuchukua nafasi ya mfungaji wa bao la kwanza kwa Majimaji, Jaffar Mohammed

86' Pato Ngonyani anaenda kugangwa nje baada ya kuumia

87' Emmanuel Martin anatoka nje, nafasi yake anachukua Geoffrey Mashiuya, matokeo bado ni 2-1

90+ Dakika 3 zimeongezwa mpira umalizike

90+ Sekunde tu zimesalia mpira umalizike

90+ Rostand amelala chini baada ya kuumia, na mpira umesimama kwa muda huku wachezaji wa Majimaji wakimlalamikia Mwamuzi kuwa anapoteza muda

Na mpira umekwisha, Yanga imeibuka mshindi wa mabao 2-1, na sasa inaingia 8 bora ya robo fainali ya Azam Sports Federation CUP.EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz