MAJIMAJI KUTUMIA KIKOSI CHA PILI KUMKABILI YANGA - EDUSPORTSTZ

Latest

MAJIMAJI KUTUMIA KIKOSI CHA PILI KUMKABILI YANGA

Image result for MAJIMAJI
Kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho siku ya kesho, kikosi cha Majimaji kitakuwa na ukosefu wa wachezaji 7 watakaoikabili Yanga.

Kocha wa timu hiyo, Habibu Kondo, amesema timu hiyo itawakosa jumla ya wachezaji saba, na sasa watalazimika kutumia wa kikosi cha pili ili waweze kupambana.

Akizungumza na ripota wa Saleh Jembe, Kondo amesema wachezaji hao wamepumzishwa kutokana na masuala mbalimbali ya kinidhamu kuwakabili.

"Itatubidi tuingize wachezaji watano wa kikosi cha pili, sababu katika kile cha kwanza, jumla ya wachezaji saba hawatokuwepo" alisema Kondo.

Kondo amewasihi mashabiki wa timu hiyo, kujitikeza kwa wingi uwanjani ili kuipa hamasa timu yao itakapoikabili Yanga kesho katika Uwanja wao wa nyumbani.

EDUSPORTSTZ inakutakia maandalizi mema ya siku. inakuomba kulike facebook page yetu au kufollow kupitia blog eneo la follow by email ili kutumiwa habari kwa wakati.
Enter your email address:


Delivered by EDUSPORTSTZ
Subscribe to EDUSPORTSTZ


Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz